Simba yapokelewa kifalme Kigoma

Mabingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Timu ya Simba, imepata mapokezi makubwa baada ya kutua mkoani Kigoma tayari kwa Fainali ya Azam Sports Federation Cup (ASFC) utakaopigwa Jumapili Uwanja wa Lake Tanganyika.

Simba imetua saa 12 jioni hapa Kigoma na kupokelewa na idadi kubwa ya mashabiki ambao wanaonekana kuwa na imani kubwa na timu yao pendwa.

Mapenzi makubwa yaliyoonyeshwa na mashabiki kwenye mapokezi ya leo yamewafanya wachezaji wetu kujiona wana deni kubwa siku ya Jumapili.

Mchezo dhidi ya Yanga tunajua utakuwa mgumu lakini  tutajipanga kuhakikisha tunawapa furaha Jumapili.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER