Simba Sports Club
News

Zimbwe Jr ampiku Kapombe Tuzo Beki Bora 2020/21

21 Oct 2021

Mlinzi wetu wa kushoto Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr' ameshinda Tuzo ya Beki Bora wa Ligi Kuu Msimu wa 2020/21 katika hafla inayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Zimbwe Jr amempiku mlinzi mwenzake wa Simba, Shomari Kapombe pamoja na mlinzi wa Yanga Dickson Job.

Advertisement

Zimbwe Jr amekuwa mhimili wetu katika idara ya ulinzi na ni miongoni mwa wachezaji waliocheza dakika nyingi msimu uliopita.

Back to homepage
Share this story