Simba Sports Club
News

Watano waitwa Taifa Stars kufuzu AFCON

6 Nov 2024

Stars ina mechi mbili muhimu ambazo ikishinda itajihakikishia tiketi ya kushiriki michuano ya AFCON ambayo itafanyika nchini Morocco Januari 2025.

Nyota hao walioitwa ni mlinda mlango Aishi Manula, walinzi Shomari Kapombe, Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr' na Abdulrazack Hamza.

Advertisement

Mwingine aliyejumuishwa kwenye kikosi hicho akiwa ni kiungo mshambuliaji, Kibu Denis.

Kikosi cha Stars kitaingia kambini kesho kujiandaa na mechi hizo ambapo ya kwanza itakuwa ugenini dhidi ya Ethiopia Novemba, 16 na kumaliza nyumbani dhidi ya Guinea Novemba, 19.

Back to homepage
Share this story