Simba Sports Club
News

Watano kupaa leo kuungana na wenzao Misri

17 Jul 2022

Juzi kikosi cha wachezaji 19 pamoja na benchi la ufundi kilitangulia Misri huku wengine wakibaki kukamilisha baadhi ya taratibu ikiwemo suala la visa.

Nyota hao ambao wataondoka leo ni mshambuliaji Moses Phiri, viungo Nassor Kapama, Taddeo Lwanga, Peter Banda na mlinzi Henock Inonga.

Advertisement

Wachezaji wengine watano ambao wapo kwenye kambi ya timu ya Taifa inayojiandaa na michuano ya CHAN wao watasubiri mpaka wamalize majukumu yao.

Kikosi chetu kitakuwa nchini Misri kwa takribani wiki tatu kabla ya kurejea nchini tayari kwa kuanza msimu mpya wa ligi 2022/23.

Back to homepage
Share this story