Simba Sports Club
News

Wachezaji wapimwa Covid-19 tayari kupaa Botswana

12 Oct 2021 By simbasc 1,045 views

Wachezaji wetu pamoja benchi la ufundi leo wamepimwa Covid-19 tayari kwa maandalizi ya safari ya kuelekea Botswana itakayokuwa Ijumaa jioni.

Kupima Covid-19 kabla ya safari kutoka nchi moja hadi nyingine ni utaratibu uliowekwa na Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) ili kudhibiti maambukizi ya ugonjwa huo.

Advertisement

Kikosi kinaelekea Botswana tayari kwa mchezo wa hatua ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Jwaneng Galax utakaopigwa Jumapili, Oktoba 17.

Tayari wachezaji waliokuwa kwenye majukumu ya timu za taifa wameanza kurejea huku wale waliokuwa Taifa Stars wakifanya mazoezi na wenzao leo.

Back to homepage
Share this story