Simba Sports Club
News

VIDEO : Timu yafanya mazoezi usiku kujiandaa na USGN

1 Apr 2022

Kikosi kimefanya mazoezi muda huu kutokana na mchezo wetu ambao utapigwa saa nne usiku hivyo taratibu za Shirikisho la Soka Afrika (CAF) linataka timu zifanye mazoezi ya mwisho katika wakati wa mechi uliopangwa.

Wachezaji wote isipokuwa Hassan Dilunga ambaye ni majeruhi wamefanya mazoezi na kila mmoja yuko tayari kwa mchezo wa Jumapili.

Advertisement

Morali ya wachezaji ipo juu na kila mmoja anafahamu umuhimu wa mchezo na yuko tayari kuipigania timu kuhakikisha tunashinda na kutinga robo fainali.

Back to homepage
Share this story