Rais Samia anatoa Sh. 5,000,000 kwa kila bao linalofungwa na wawakilishi wa nchi kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa na Shirikisho ili kuongeza morali.
Msigwa amemkabidhi kitita hicho Meneja Habari na Mawasiliano wa klabu, Ahmed Ally ambaye muda huo huo alimpatia nahodha John Bocco ili akagawane na wachezaji wenzake.