Simba Sports Club
News

Uongozi wakutana na benchi la ufundi na wachezaji

13 Sep 2025

Miongoni mwa vitu vilivyojadiliwa ni malengo kuelekea msimu mpya wa mashindano na nini kinatakiwa kufanyika kutoka kwa benchi la ufundi na wachezaji.

Pia katika Mkutano huo Viongozi wamewakumbusha wachezaji kuhakikisha wanafuata makubaliano ya mikataba waliyosaini na klabu ili kuondoa migogoro ambayo haina lazima.

Advertisement

Aidha Viongozi wameweka wazi kuwa kila mchezaji anatakiwa kuhakikisha anapigania nembo ya klabu kila atakapopata nafasi ya kucheza kwakuwa tunahitaji kufikia malengo.

Wakati huo huo malengo yetu kama klabu yanabaki yale yake kama ilivyokuwa msimu uliopita kupambania kupata mataji yote ya ndani na kufanya vizuri katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Back to homepage
Share this story