Simba Sports Club
News

Tutacheza mechi mbili kabla ya kupisha AFCON

1 Dec 2025

Kikosi kinatarajia kurejea nchini kesho kutoka Mali na moja kwa moja kitaingia kambini kujiandaa na mchezo wa Ligi dhidi ya Mbeya City.

Mchezo dhidi ya City utapigwa Alhamisi, Disemba 4 katika Uwanja wa Meja Jenerali Michael Isamuhyo saa moja usiku tukiwa sisi wenyeji.

Advertisement

Mechi ya pili itakuwa dhidi ya Azam FC ambayo itapigwa Disemba 7 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa saa 11 jioni.

Baada ya mechi hizo ligi itasimama kwa mwezi mzima kupisha michuano ya AFCON ambayo itaanza kutimua vumbi Disemba 21 nchini Morocco.

Back to homepage
Share this story