Simba Sports Club
News

Tunawatakia kheri wachezaji wetu kwenye michuano ya AFCON

17 Jan 2024

Wachezaji wetu wote mataifa yao matatu yapo katika kundi moja, Kundi F.

Aishi Manula, Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr' Mzamiru Yassin na Kibu Denis watawakilisha Tanzania 'Taifa Stars' katika mchezo dhidi ya Morocco ambao utaanza saa mbili usiku.

Advertisement

Henock Inonga ataiwakilisha DR Congo katika mchezo dhidi ya Zambia anayochezea kiungo wetu mshambuliaji, Clatous Chama utakaopigwa saa tano usiku.

Simba inawatakia kheri wachezaji wote sita kuwa na mchezo mzuri na kusaidia mataifa yao kufanya vizuri.

Back to homepage
Share this story