Simba Sports Club
News

Tumezindua rasmi jezi zetu Msimu wa 2022/23

7 Aug 2022

Jezi zetu zipo kwenye ubora mkubwa kuanzia zilivyotengenezwa kimwonekano

Jezi zilizozinduliwa ziko aina tatu kama kawaida yaani ya nyumbani (nyekundu), ugenini (nyeupe) na jezi namba tatu (kijivu).

Advertisement

Baada ya uzinduzi huu wa jezi zitaanza kuuzwa katika maduka yote ya Vunjabei nchi nzima ambapo Wanasimba wataenda kununua kwa ajili ya mtoko husani wa kesho kwenye Tamasha letu la Simba Day.

Tunawaomba Wanasimba kununua jezi kwa wingi ili kesho kwenye Tamasha letu pale Benjamin Mkapa tupendeze kama kawaida yetu.

Back to homepage
Share this story