Simba Sports Club
News

Tumetinga Robo Fainali CRDB Federation Cup

27 Mar 2025

Joshua Mutale alitupatia bao la kwanza dakika ya 15 kwa shuti la mguu wa kushoto akiwa ndani ya 18 baada ya kumalizia mpira wa krosi uliopigwa na Valentine Nouma.

Leonel Ateba alitupatia bao la pili kwa mkwaju wa penati dakika ya 30 kufuatia Elie Mpanzu kufanyiwa madhambi ndani ya 18.

Joseph Mussa aliwapatia Bigman bao la kwanza dakika ya 45 kwa shuti nje ya 18 baada ya kuwazidi ujanja walinzi wetu.

Advertisement

Kipindi cha pili tulitengeneza nafasi kadhaa za kufunga lakini Bigman walikuwa makini kuhakikisha hawafanyi makosa ambayo yangewagharimu.

X1: Abel, Kijili (Chamou 62') Duchu, Kazi, Ngoma, Mpanzu (Chasambi 40'), Deborah (Okajepha 81') Ateba (Mukwala 81'), Ahoua (Awesu 81'), Mutale

Walioonyeshwa kadi: Kazi 45'

Back to homepage
Share this story