CAF imekuwa na utaratibu wa kuruhusu idadi chache ya mashabiki kwa sababu ya tahadhari juu ya ugonjwa wa Covid-19.
Hii ni mara ya kwanza baada ya kupita muda mrefu kuruhusiwa kujaza uwanja tangu lilipoingia janga la ugonjwa huo.
Viingilio vimetangazwa kama ifuatavyo:
VIP A Sh 30,000
Advertisement
VIP B Sh 20,000
VIP C Sh 10,000
Mzunguko Sh 3,000
Tiketi zimeanza kuuzwa leo kupitia mitandao ya simu na lengo letu ni kuhakikisha tunaujaza uwanja ili Orlando wavute pumzi ya moto.