Mchezo ulianza kwa kasi ya kadiri timu zikishambuliana kwa zamu ambapo dakika ya 13 alimanusura Habib Kyombo atupatie bao baada ya kuushindwa kumalizia pasi ya Augustine Okrah.
Prince Dube aliwapatia Azam bao hilo pekee dakika ya 34 akimalizia pasi ya James Akaminko na kupiga shuti lililomshinda mlinda mlango Aishi Manula.
Advertisement
Dakika 15 za kwanza za kipindi cha pili Azam walikaa nyuma zaidi kujilinda wakituacha tucheze huku wakifanya mashambulizi machache ya kushtukiza.
Kocha Juma Mgunda aliwatoa Kyombo, Okrah, Jonas Mkude na Nassor Kapama kuwaingiza John Bocco, Peter Banda, Kibu Denis na Pape Sakho.