Simba Sports Club
News

Tumepata pointi tatu kwa KVZ

5 Jan 2023

Mchezo ulianza kwa kasi ya kawaida ukichezwa zaidi katikati ya uwanja huku tukishambuliana kwa zamu lakini tulimiliki sehemu kubwa ya mchezo.

Mshambuaji Michael Joseph alitupatia bao hilo pekee kwa kichwa dakika ya 40 baada ya kumalizia mpira wa krosi uliopigwa na Augustine Okrah.

Kipindi cha pili hakukuwa na mabadiliko makubwa ambapo tuliendelea kulishambulia lango la KVZ lakini bado tulikosa utulivu.

Advertisement

Kocha Juma Mgunda alifanya mabadiliko ya mchezo mmoja ambapo alimtoa Nelson Okwa na kumuingiza Joseph Mbaga.

Katika mchezo huo mfungaji wa bao pekee Joseph Michael ameibuka mchezaji bora na kukabidhiwa kitita cha Sh. 500,000 kutoka kwa wadhamini.

Back to homepage
Share this story