Simba Sports Club
News

Tumepata pointi tatu Ali Hassan Mwinyi

6 Feb 2024 By simbasc 1,607 views
Kikosi chetu kimefanikiwa kuibuka na ushindi wa mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Tabora United katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora. Pa Omar Jobe alitupatia bao la kwanza kwa kichwa dakika ya 19 baada ya kumalizia mpira wa adhabu uliopigwa na Clatous Chama. Sadio Kanoute alitupatia bao la pili kwa kichwa dakika ya 36 baada ya kumalizia mpira wa krosi uliopigwa na Shomari Kapombe. Che Malone alitupatia bao la tatu dakika ya 59 akiwa ndani ya 18 baada ya kumalizia pasi ya Chama. Fred Michael alitupatia bao la nne dakika ya 88 baada ya kumzidi ujanja mlinzi wa Tabora na kupiga shuti lililomshinda mlinda mlango John Noble. X1: Noble, Maulid, Mbatty, Lulihoshi, Bikoko, Milandui, Mbombo, Najim, Okutu, Lambele, Nakibinge Walioonyeshwa kadi: Nakibinge 56' Lolihoshi 65' X1: Lakred, Kapombe, Zimbwe Jr, Kennedy, Che Malone, Babacar (Duchu 85') Kibu (Balua 85'), Kanoute (Mzamiru 69'), Jobe (Fred 69'), Ntibazonkiza (Miqussone 75'), Chama Walioonyeshwa kadi: Kanoute 41'
Advertisement
Back to homepage
Share this story