Simba Sports Club
News

Tumepata alama moja Songea

29 Jun 2022

Mchezo ulianza kwa kasi timu zikishambuliana kwa zamu lakini ulikuwa unachezwa zaidi katikati ya uwanja kwa ufundi mkubwa.

Mlinda mlango wetu Beno Kakolanya aliokoa mipira kadhaa iliyokuwa ya hatari wakati Kibu Denis akipoteza nafasi za kufunga ambazo zingetufanya kwenda mapumziko tukiwa mbele.

Advertisement

Kipindi cha pili tuliongeza kasi ya kutafuta bao la ushindi lakini tulikosa umakini katika eneo la mwisho na mashambulizi yakaishia kwa mlinda mlango wa Mbeya Kwanza.

Kocha Seleman Matola aliwatoa Kassim Omary na Yusuf Mhilu na kuwaingiza Henock Inonga na John Bocco.

Back to homepage
Share this story