Simba Sports Club
News

Tumepangwa na TRA 32 bora ASFC

2 Feb 2024 By simbasc 318 views
Droo ya hatua ya 32 bora ya michuano ya Azam Sports Federation Cup (ASFC) imekamilika na tumepangwa kucheza na timu ya TRA FC kutoka Kilimanjaro. Tumefika hatua hii baada ya kufanikiwa kuifunga Tembo FC kutoka Tabora kwa mabao 4-0 katika mchezo uliopigwa juzi Jumatano Uwanja wa Azam Complex, Chamazi. Mchezo wetu dhidi ya TRA unatarajiwa kufanyika kati ya Februari 20 hadi 22 ambapo sisi ndio tutakuwa wenyeji. Malengo yetu ni msimu huu ni kuhakikisha tunashinda taji la kila mashindano ambayo tutashiriki.
Advertisement
Back to homepage
Share this story