Mchezo huo utapigwa kati ya Aprili 8-13 ambapo sisi ndiyo tutakuwa wenyeji hivyo mtanange utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Mshindi kati yetu na Pamba atakutana na mshindi wa Yanga na Geita Gold katika mchezo wa Nusu Fainali.
Advertisement
Sisi ndiyo mabingwa watetezi wa michuano hii na moja ya lengo letu msimu huu ni kuhakikisha tunatetea taji letu.