Simba Sports Club
News

Tumepangwa na Al Masry Robo Fainali Shirikisho

20 Feb 2025

Tutaanzia ugenini mchezo wa kwanza utapigwa kati ya Aprili 1-2 huku mechi ya marudiano ikipigwa kati ya Aprili 8-9.

Tumewahi kukutana na Al Masry kwenye michuano hii ambapo tulipokutana mwaka 2018.

Advertisement

Katika mchezo wa mkondo wa kwanza tukiwa nyumbani tulitoka sare ya mabao 2-2 na mechi ya marudiano nchini Misri ikamalizika kwa sare ya bila kufungana.

Back to homepage
Share this story