Simba Sports Club
News

Tumepangwa na Ahly Robo Fainali Mabingwa Afrika

12 Mar 2024

Mchezo wa mkondo wa kwanza utapigwa kati ya Machi 29 na 30 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa huku ule wa marudiano ukipigwa kati ya Aprili 5 na 6 jijini Cairo.

Msimu huu tumekutana na Al Ahly katika michuano mipya ya African Football League (AFL) ambapo miamba hiyo pia ilitutoa kwa faida ya bao la ugenini.

Advertisement

Mshindi wa jumla kati yetu na Al Ahly atakutana na mshindi kati ya TP Mazembe na Petro De Luanda ya Angola.

Back to homepage
Share this story