Pape Sakho alitupatia bao la kwanza dakika ya 16 baada ya kumalizia pasi ya kisigino iliyopigwa na Kibu Denis.
Peter Banda alitupatia bao la pili dakika ya 44 baada ya kupiga shuti lililokwenda moja kwa moja na kumshinda mlinda mlango wa Mtibwa, Shaban Kado.
Advertisement
Kiungo wa Mtibwa Said Ndemla alitolewa kwa kuonyeshwa kadi nyekundu dakika ya 66 baada ya kumchezea vibaya Sadio Kanoute.
Kocha Seleman Matola alifanya mabadiliko ya kuwatoa Denis Kibu na Pape Sakho na Kuwaingiza Yusuf Mhilu na Taddeo Lwanga.