Rais Samia amekuwa akitoa kiasi hicho cha pesa kwa kila bao tunalofunga kwenye michuano hii ili kuongeza morali kwa timu za Tanzania kufanya vizuri.
Pesa hiyo amekabidhiwa nahodha, John Bocco na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Akson ambaye alikuwa Mgeni Rasmi wa mchezo wetu.
Advertisement
Katika mchezo uliopita wa nyumbani dhidi ya Horoya kutoka Guinea tulikabidhiwa Sh. 35,000,000 baada ya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 7-0.