Simba Sports Club
News

Tumeingiza mguu mmoja Nusu Fainali Shirikisho

17 Apr 2022

Tulianza mchezo kwa kasi kwa kuliandama lango la Orlando na kumiliki sehemu kubwa kwa kutengeneza nafasi lakini ufanisi wetu haukuwa mzuri.

Orlando walicheza kwa kujilinda zaidi wakijaza watu wengi katika eneo lao huku wakifanya mashambulizi machache ya kushtukiza.

Mlinzi wa kulia Shomari Kapombe alitupatia bao la kwanza kwa mkwaju wa penati dakika ya 68 baada ya Bernard Morrison kufanyiwa madhambi ndani ya 18.

Advertisement

Kocha Pablo Franco aliwatoa Peter Banda, Taddeo Lwanga, Morrison, Pape Sakho na Chris Mugalu kuwaingiza Kibu Denis, Rally Bwalya, Mzamiru Yassin, Yusuf Mhilu na Medie Kagere.

Kutokana na hatua hiyo, kwa sasa tutahitaji ushindi au sare ya aina yoyote katika mchezo wa marudiano utakaofanyika nchini Afrika Kusini ili tufuzu nusu fainali.

Back to homepage
Share this story