Simba Sports Club
News

Tumegawana pointi na Yanga

30 Apr 2022

Mchezo ulianza kwa kasi ya kawaida timu zikicheza soka la mbinu na kusomana huku mpira ukichezwa zaidi katikati ya uwanja.

Makipa wa timu zote hawakupata misukosuko kipindi cha kwanza kutokana na idadi chache ya mashambulizi yaliyotengenezwa.

Advertisement

Kipindi cha pili tuliongeza kasi kidogo na kutengeneza nafasi kadhaa za kufunga lakini hata hivyo hatukuzitumia ipasavyo.

Kocha Pablo aliwatoa Clatous Chama, Sadio Kanoute, Bernard Morrison na Pape Sakho na kuwaingiza Rally Bwalya, Mzamiru Yassin, Kibu Denis na John Bocco.

Back to homepage
Share this story