Simba Sports Club
News

Tumefanya Mazoezi ya mwisho CCM Kirumba

11 Feb 2024 By simbasc 913 views
Kikosi chetu kimefanya mazoezi ya mwisho katika Uwanja wa CCM Kirumba kujiandaa na mchezo wa kesho wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Geita Gold. Wachezaji wote wameshiriki mazoezi hayo na wapo kwenye hali nzuri tayari kwa mchezo wa kesho. Tunategemea kupata upinzani mkubwa kutoka kwa Geita lakini hata hivyo tumejipanga kuhakikisha tunaondoka na alama zote tatu. Hakuna mchezaji yoyote ambaye tutamkosa katika mchezo wa kesho kutokana nakuwa majeruhi au kutumikia adhabu ya kadi hivyo tupo kamili kuivaa Geita kesho.
Advertisement
Back to homepage
Share this story