Simba Sports Club
News

Tulipotoka hadi kufika Nusu Fainali ASFC

7 May 2023 By simbasc 214 views
Kikosi chetu leo saa 9:30 Alasiri kitashuka katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona kuikabili Azam FC katika mchezo wa nusu fainali ya Azam Sports Federation Cup (ASFC). Kabla ya mchezo wa leo tumecheza mechi nne ambazo zimetupa tiketi ya kukutana na Azam kwenye mechi ya nusu fainali. Safari yetu ilipoanzia Hadi kufika leo..... Hatua ya 64............ Simba 8-0 Eagle FC Mchezo wetu wa kwanza wa ASFC ulikuwa dhidi ya Eagle FC uliopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Disemba 10, 2022 ambao ulikuwa hatua ya 64 bora na tulishinda mabao 8-0. Mabao yetu yalifungwa na Moses Phiri ⚽⚽⚽⚽ Clatous Chama ⚽⚽ Habib Kyombo ⚽ Pape Sakho ⚽ Hatua ya 32............... Simba 1-0 Coastal Union Mchezo wetu wa hatua ya 32 bora dhidi ya Coastal Union ulipigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Januari 28, 2022 na tulifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao moja. Bao letu lilifungwa na Sadio Kanoute ⚽ Hatua ya 16................ Simba 4-0 African Sports Mchezo wetu wa hatua ya 16 bora ulipigwa Machi 2, 2023 katika Uwanja wa Uhuru na tuliibuka na ushindi wa mabao 4-0. Mabao yetu yalifungwa na Jean Baleke ⚽ Kennedy Juma ⚽ Mohamed Mussa ⚽ Jimmyson Mwanuke ⚽ Robo fainali...................... Simba 5-1 Ihefu Mchezo wetu wa robo fainali uliopigwa katika Uwanja wa Azam Complex, Aprili 7, 2023 na tuliibuka na ushindi wa mabao 5-1. Mabao yetu yalifungwa na Jean Baleke ⚽⚽⚽ Saido Ntibazonkiza ⚽ Pape Sakho ⚽ N.B Mpaka tunaingia kwenye mchezo wa leo wa nusu fainali tayari tumefunga mabao 18 tukiwa tumeruhusu bao moja.
Advertisement
Back to homepage
Share this story