Kikosi kimeondoka jijini Dar es Salaam asubuhi kwa usafiri wa treni ya Mwendokasi SGR na kupitia Dodoma kabla ya kuchukua basi mpaka Tabora.
Baada ya kuwasili Tabora saa 11 kikosi kitafanya mazoezi ya mwisho katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi kujiweka sawa kabla ya kushuka dimbani kesho.