Simba Sports Club
News

Timu yawasili salama Kagera

19 Dec 2022

Kikosi kimetokea jijini Mwanza baada ya kufanikiwa kuibuka na ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Geita Gold jana katika Uwanja wa CCM Kirumba.

Timu imeondoka kikosi kizima cha wachezaji 24 ambao tuliosafiri nao kutoka jijini Dar es Salaam kamili kwa ajili ya mchezo wa Jumatano.

Advertisement

Baada ya kuwasili wachezaji watapata muda wa kupumzika kidogo na baadae watafanya mazoezi ya utimamu wa mwili kujiweka sawa.

Kesho saa moja usiku kikosi kitafanya mazoezi ya mwisho katika Uwanja wa Kaitaba kabla ya kushuka dimbani keshokutwa Jumatano.

Back to homepage
Share this story