Simba Sports Club
News

Timu yawasili Salama FrancisTown

18 Sep 2025

Kikosi kimefika jana nchini Botswana lakini leo kimewasili katika mji wa FrancisTown kutakapochezwa mchezo wetu.

Baada ya kufika FrancisTown Kikosi chetu kimefanya mazoezi ya utimamu wa mwili kutokana na uchovu wa safari.

Advertisement

Kesho jioni Kikosi kitafanya mazoezi ya mwisho katika uwanja Obedi Itani Chilume ambao ndio tutautumia katika mchezo wetu wa Jumamosi.

Back to homepage
Share this story