Kikosi kiliondoka jijini Dar es Salaam alfajiri kikipitia Ethiopia kabla ya kuunganisha hadi hapa Angola.
Baada ya kikosi kufika kimeelekea hotelini ili wachezaji waweze kupumzika kwa saa chache kabla ya kufanya mazoezi ya utimamu baada ya safari ndefu.
Advertisement
Kocha Mkuu Fadlu Davids ataendelea na programu ya mazoezi kesho pamoja na keshokutwa kabla ya Jumapili kushuka dimbani.