Kikosi kimewasili mchana na wachezaji wamepata saa kadhaa za kupumzika na jioni wamefanya mazoezi ya utimamu wa mwili.
Hali ya hewa ni joto sawa na jijini Dar es Salaam hivyo wachezaji hawatapata changamoto ya kuzoea mazingira.
Advertisement
Kesho kikosi kitaendelea na programu ya mazoezi na keshokutwa kitafanya ya mwisho kabla ya kuivaa Petro De Luanda siku ya Jumamosi.
Morali za wachezaji zipo juu na wachezaji wote waliosafari wapo kwenye hali nzuri.