Simba Sports Club
News

Timu yatua salama nchini Benin

18 Mar 2022 By simbasc 1,358 views

Kikosi chetu kimewasili salama nchini Benin mchana huu tayari kwa mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya ASEC Mimosas utakaopigwa Jumapili saa moja usiku katika Uwanja wa Generali Mathieu Kérékou.

Baada ya kikosi kufika wachezaji watapumzika kwa saa chache kabla ya kwenda mazoezini jioni kuweka miili sawa (recovery).

Advertisement

Tutaingia katika mchezo Jumapili tukiwa na lengo la kutafuta alama tatu muhimu ili kujihakikishia nafasi ya kuingia robo fainali ya michuano hii.

Back to homepage
Share this story