Timu iliondoka jana jioni ikiwa na kikosi cha watu 30 ambapo mazoezi rasmi yataanza kesho baada ya Kocha Mkuu kufika.
Kundi la pili la wachezaji pamoja na sehemu ya benchi la ufundi litawasili kesho na kujiunga pamoja na kuendelea na Pre Season.
Advertisement
Ikiwa Misri timu inatarajia kucheza mechi kadhaa za kirafiki ili kulipa benchi la ufundi nafasi ya kuona jinsi gani wachezaji wanashika mafunzo wanayowapa.
Timu itakuwa nchini Misri kwa wiki tatu kabla ya kurejea jijini Dar es Salaam Julai 31.