Baada ya kikosi kurejea wachezaji wamepewa mapumziko ya kwenda kukutana na familia zao kabla ya kuanza maandalizi mchezo wa marudiano utakaopigwa Jumapili ijayo Uwanja wa Benjamin Mkapa saa 10 jioni.
Kesho kikosi kitaanza mazoezi katika Uwanja wa Mo Simba Arena na Jumatano kitaingia kambini moja kwa moja kujiandaa na mtanange huo muhimu ambao utatupa kibali cha kuingia hatua ya makundi.