Kikosi kimeondoka Tanga mchana baada ya kufanya mazoezi ya utimamu wa mwili ili kuwaweka wachezaji sawa kabla ya kuanza safari.
Baada ya kufika wachezaji wameruhusiwa kwenda kupumzika na kesho mchana kikosi kitaingia kambini kujiandaa na mchezo dhidi ya Singida Fountain Gate utakaopigwa Jumanne saa moja usiku Uwanja wa Azam Complex.
Advertisement
Kikosi kitafanya mazoezi ya mwisho katika Uwanja wetu wa Mo Simba Arena tayari kwa kuwavaa Singida.