Simba Sports Club
News

Timu yarejea mazoezini, Kuifuata Prisons Jioni

3 Oct 2023

Mazoezi hayo yamefanyika katika Uwanja wetu wa Mo Simba Arena chini ya Kocha Mkuu, Roberto Oliviera 'Robertinho' na wasaidizi wake baada ya mapumziko ya siku ya siku moja.

Baada ya mazoezi hayo wachezaji watapumzika kwa saa chache kabla ya leo jioni kuaanza safari ya kuelekea jijini Mbeya tayari kwa mchezo.

Advertisement

Kesho timu itafanya mazoezi ya mwisho kabla ya kushuka dimbani Alhamisi.

Tunatarajia kusafiri na kikosi kamili kwa ajili ya mchezo huo kwakuwa lengo letu ni kuhakikisha tunarudi na alama tatu ugenini.

Back to homepage
Share this story