Baada ya mapumziko kupisha michuano ya FIFA Series wachezaji walipewa mapumziko na machi 27 walirejea mazoezini na leo wameingia kambini rasmi.
Wachezaji wote wameingia kambini na wapo kwenye hali nzuri kuelekea mchezo huo ambao ni tunategemea utakuwa mgumu.
Advertisement
Kesho jioni kikosi kitafanya mazoezi ya mwisho kabla ya Alhamisi kushuka dimbani kwa ajili ya kusaka alama tatu muhimu nyumbani.
Mchezo wetu dhidi ya Coastal Union utapigwa Alhamisi saa moja usiku katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo.