Wachezaji wote wameshiriki mazoezi hayo na hakuna yoyote ambaye amepata maumivu yatakayomfanya kukosa mchezo wa kesho.
Baada ya mchezo wa juzi wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Raja Casablanca juzi, jana tumeanza maandalizi ya mchezo dhidi ya Azam moja kwa moja na lengo ni kuhakikisha tunashinda.
Viingilio vya mchezo ni kama ifuatavyo:
Mzungo Sh. 5000
Advertisement
VIP B na C na Sh. 10,000
VIP A Sh. 15,000
Kama kawaida mchezo wetu wa kesho utapigwa Benjamin Mkapa saa moja usiku.