Simba Sports Club
News

Timu yaifuata Mbeya Kwanza Songea

27 Jun 2022

Kikosi kimeondoka jijini Mbeya baada ya mchezo wa jana kwa basi kikiwa na wachezaji wote tuliosafiri nao kwa ajili ya mechi mbili za Nyanda za Juu Kusini.

Baada ya timu kuwasili Songea wachezaji watafanya mazoezi ya utimamu wa mwili (recovery) baada ya mechi ya jana dhidi ya Tanzania Prisons na kesho tutafanya ya mwisho.

Advertisement

Mchezo wetu dhidi ya Mbeya Kwanza utapigwa Jumatano saa 10 jioni katika Uwanja wa Majimaji.

Back to homepage
Share this story