Baada ya mchezo wa jana dhidi ya Prisons wachezaji wamefanya mazoezi ya utimamu wa mwili katika Uwanja wa Highland na mchana kitaelekea Tanga.
Kikosi kitafanya mazoezi ya mwisho kesho jioni katika Uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga tayari kwa mchezo wa Jumamosi.