Morali ya wachezaji ipo juu kuelekea mchezo wa kesho kila mmoja amejitahidi kufanya vizuri mazoezini ili kulishawishi benchi la ufundi kumpa nafasi kwenye mechi ya kesho.
Tunajua mchezo utakuwa mgumu na tunaiheshimu Yanga lakini tunahitaji zaidi ushindi ili tutinge fainali ya michuano hii ambayo sisi ni mabingwa watetezi.
Advertisement
Mchezo wa kesho utaanza saa 9:30 alasiri katika Uwanja wa CCM Kirumba.