Wachezaji wote tuliosafiri nao wameshiriki mazoezi hayo na wapo kwenye hali nzuri na hakuna ambaye atakosekana kutokana na kupata maumivu.
Katika mazoezi hayo kila mchezaji ameonekana kuonyesha jitihada kubwa akiwa na ari ya hali juu tayari kwa mchezo huo ambao unasubiriwa kwa hamu kubwa.
Advertisement
Kocha mkuu Steve Barker na wasaidizi wake wamekuwa wakiwasisitiza wachezaji kuwa watulivu na kutokuwa na presha badala yake wajiamini kwakuwa wana uwezo mkubwa wa kuiwezesha timu kupata ushindi.