Simba Sports Club
News

Timu yafanya mazoezi ya mwisho Mo Arena kujiandaa na Ihefu

11 Nov 2022

Baada ya kikosi kurejea jijini Dar es Salaam jana kutoka mkoani Singida kiliingia kambini moja kwa moja tayari kuanza maandalizi ya mchezo wa kesho.

Wachezaji wote wamefanya mazoezi isipokuwa Peter Banda aliyepata majeraha kwenye mchezo uliopita na wale majeruhi wa muda mrefu Jimmyson Mwanuke na Israel Patrick.

Advertisement

Ingawa Ihefu ipo mwisho kwenye msimamo lakini hatuwadharau na tutaingia kwa tahadhari zote kwa kuwa tunahitaji kupata alama tatu nyumbani.

Morali ya wachezaji ipo juu na wamefanya jitihada mazoezini ili kulishawishi benchi la ufundi kuwapa nafasi kwenye mchezo wa kesho.

Back to homepage
Share this story