Simba Sports Club
News

Timu yafanya mazoezi ya mwisho Mo Arena

24 Sep 2024

Wachezaji wote wameshiriki mazoezi hayo kikamilifu na hakuna yeyote ambaye amepata maumivu ambayo yatamfanya kuukosa mchezo huo.

Kikosi kitaondoka kesho kikiwa na wachezaji 22 tayari kwa mchezo huo ambao utapigwa katika Uwanja wa New Amaan Complex Alhamisi saa 2:30 usiku.

Advertisement

Mchezo huo utakuwa ni wa kwanza wa Ligi Kuu ya NBC kupigwa Zanzibar nasi tumejipanga kuhakikisha tunaanza kwa ushindi.

Tunaondoka tukiwa na kumbukumbu ya ushindi mnono wa mabao 3-1 tuliopata dhidi ya Al Ahli Tripoli ambao umetuwezesha kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Back to homepage
Share this story