Wachezaji wote wamefanya mazoezi hayo na wapo kwenye hali nzuri kuelekea mchezo wa kesho ambao ni wakutafuta mshindi wa tatu wa Ngao ya Jamii.
Morali za wachezaji zipo juu na kila mmoja yupo tayari kuipambania timu kama atapata nafasi ya kucheza.
Advertisement
Kocha Fadlu Davids ameweka wazi kuwa tunaupa umuhimu mkubwa na tutaingia kwenye mchezo wa kesho kwa lengo la kutafuta ushindi.