Simba Sports Club
News

Timu yafanya mazoezi ya mwisho Mbweni

27 Dec 2023 By simbasc 577 views
Kikosi chetu cha Simba Queens kesho saa 10 jioni kitashuka katika Uwanja wa Azam Complex kuikabili Baobab Queens kutoka Dodoma katika mchezo wa pili wa ligi kuu soka ya Wanawake msimu wa 2023/2024. Kikosi kipo tayari kwa ajili ya mchezo na leo asubuhi kimefanya mazoezi ya mwisho katika Uwanja wa Mbweni Veterani kujiandaa na mchezo huo. Tunawaheshimu Baobab na tunajua utakuwa mchezo mgumu kini tumejipanga kuhakikisha tunashinda na kuchukua alama zote tatu.
Advertisement
Back to homepage
Share this story