Simba Sports Club
News

Timu yafanya mazoezi ya mwisho Mao Tse-tung

2 Jan 2023 By simba 296 views
  Kikosi chetu leo jioni kimefanya mazoezi ya mwisho katika Uwanja wa Mao Tse-tung kujiandaa na mchezo wa kwanza wa Michuano ya Mapinduzi dhidi ya Mlandege. Kesho saa 2:15 usiku tutashuka katika Uwanja wa Amani kuanza kutetea taji letu ambalo tulilitwaa mwaka jana. Kikosi kimewasili hapa Zanzibar leo jioni ambapo wachezaji walipewa muda wa kupumzika kabla ya kwenda mazoezini kujiandaa na Mlandege. Wachezaji wote wameshiriki mazoezi hayo na wapo kwenye hali nzuri tayari kwa mchezo wa kesho.
Advertisement
Back to homepage
Share this story