Mazoezi hayo ambayo yamesimamiwa na Kocha Mkuu, Roberto Oliviera 'Robertinho' na wasaidizi wake yamefanyika katika Uwanja wa Sokoine ambao tutautumia kesho kwenye mchezo.
Wachezaji wote 22 tuliosafiri nao wameshiriki mazoezi hayo kikamilifu na hakuna aliyepata maumivu ambayo yatamfanya kuukosa mchezo wa kesho.
Advertisement
Morali za wachezaji zipo juu na kila mmoja ameonyesha jitihada mazoezini ili kulishawishi benchi la ufundi kumpa nafasi ya kucheza kesho.