Mazoezi hayo yamefanyika usiku muda ambao mchezo huo utapigwa ambapo kwa Libya itakuwa ni saa moja na nyumbani Tanzania itakuwa ni saa mbili usiku.
Wachezaji wote wameshiriki mazoezi hayo na wapo kwenye hali nzuri tayari kwa mchezo huo ambao tunaamini utakuwa mgumu.
Advertisement
Morali za wachezaji zipo juu na kila mmoja amejitahidi kuonyesha uwezo kwa walimu ili kupata nafasi ya kuanza kwenye mchezo wa kesho.