Simba Sports Club
News

Timu yafanya mazoezi ya mwisho Libya

14 Sep 2024

Mazoezi hayo yamefanyika usiku muda ambao mchezo huo utapigwa ambapo kwa Libya itakuwa ni saa moja na nyumbani Tanzania itakuwa ni saa mbili usiku.

Wachezaji wote wameshiriki mazoezi hayo na wapo kwenye hali nzuri tayari kwa mchezo huo ambao tunaamini utakuwa mgumu.

Advertisement

Morali za wachezaji zipo juu na kila mmoja amejitahidi kuonyesha uwezo kwa walimu ili kupata nafasi ya kuanza kwenye mchezo wa kesho.

Back to homepage
Share this story